MOROGORO: Ajali mbaya, Bus limegonga treni, Mwanafunzi 1 afariki
MOROGORO: Ajali mbaya, Bus limegonga treni, Mwanafunzi 1 afariki
Asubuhi hii ya sasa hivi kuna ajali mbaya sana imetokea ya treni katika eneo la TANESCO pale Morogoro mjini ambapo Coaster iliyobeba wanafunzi wengi wa Shule ya sekondari ya Kayenzi na raia wachache kadhaa imegonga treni.
Inasemekana wanafunzi watatu wamefariki, miili imetapakaa eneo la tukio, pia majeruhi kadhaa wamepatikana.
Wenye ndugu wanafunzi wa shule hiyo ambao ni wakazi wa Morogoro mjini, fuatilieni tukio hili.
Chanzo: Nimepigiwa na simu na mtu wangu wa karibu kutoka eneo la tukio
Inna Lilah Waina Lilah Raj'un.
====
UPDATES: Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa, Frank Jacob amethibitisha kifo cha Mtu mmoja(Mwanafunzi) katika ajali iliyohusisha basi la Wanafunzi na Treni mapema leo.
No comments:
Post a Comment