CHEICK TIOTE AFARIKI DUNIA AKIWA UWANJANI
Cheick Tiote: Mchezaji wa zamani wa Newcastle afariki dunia

Alihamia klabu ya Beijing Enterprises mwezi Februari.
"Ni kwa huzuni kubwa ambapo ninathibitisha kwamba Cheick Tiote alifariki mapema leo baada ya kuzimia wakati wa mazoezi," msemaji wake alisema.
"Hatuwezi kusema zaidi kwa sasa na tunaomba kwamba familia yake iheshimiwe kipindi hiki kigumu. Tunaomba maombi yenu."
Tiote alizaliwa Ivory Coast na alikuwa kwenye kikosi kilichoshinda Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.
No comments:
Post a Comment