[TRENDING][10]

CENTER OF ICT
ENTERTAINMENT
GOSSIP
NEWZ
SPORTS
VIDEOS

Tetesi za Soka Ulaya Alhamisi

Tetesi za Soka Ulaya Alhamisi

Antonio Conte
Meneja wa Chelsea Antonio Conte bado anaungwa mkono na bodi licha ya kipigo walichopata kutoka Roma siku ya Jumanne. (Mirror)
Everton wako tayari kulipa pauni milioni 2.5 za kuachiliwa meneja wa Burnley Sean Dyche. (Sun)
Ronald KoemanHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRonald Koeman
Nuno Espirito Santo anatathmini ikiwa atachukua nafasi iliyo Everton kufuata kufutwa kwa Ronald Koeman, lakini pia anatarajiwa kusalia Wolverhampton Wanderers. (Guardian)
Aliyekuwa meneja wa Rangers Ally McCoist, anapania kuongoza Sunderland kufuatia kufutwa kwa meneja Simona Grayson. (Daily Star)
Mshambuliaji wa Gremio, Luan, 24, ambaye alikuwa akitafutwa na Barcelona, Liverpool na Arsenal amesaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Brazil hadi mwaka 2010. (Goal)
Jose MourinhoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJose Mourinho
Mameneja Mauricio Pochettino wa Tottenham, Antonio Conte wa Chelsea na Jose Mourinho wa Manchester United huenda wakawa kwenye orodha ya wale wanaosakwa na Paris St-Germain. (Paris United - in French)
Barcelona wana matumaini ya kumsajili mshambuliaji Timo Wener, 21, na mlinzi Dayot Upamecano, 19, kutoka RB Leipzig. (Mundo Deportivo via
Meneja wa Southend, Phil Brown anasema kuchukua usukani huko Sunderland inaweza kutumiza ndoto yake (Basildon, Canvey and Southend Echo)
Arsene WengerHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionArsene Wenger
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger, amekana uvumi wa kuihusisha Arsenal na kuhama kwa wing'a wa Monaco Thomas Lemar. (Evening Standard)
Wenger anataka kukamilisha mazungumzo ya mkataba na mchezaji wa kiungo cha kati, Jack Wilshere, ifikapo Disemba. (Mirror)

About Author Mohamed Abu 'l-Gharaniq

when an unknown printer took a galley of type and scrambled it to make a type specimen book. It has survived not only five centuries.

No comments:

Post a Comment

Start typing and press Enter to search